WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Monday 2 March 2015

WAZIRI MKUU INDIA ATAKA SULUHU ZA USALAMA MTANDAO KWA WANA TEHAMA

Baada ya miaka 25 ya mafanikio nchini india katika sekta ya TEHAMA, Waziri mkuu wa nchi hiyo amezitaka sekta za TEHAMA kuboresha usalama wa mitandao ili kukabiliana na wimbi la uhalifu mtandao kwa kuwa na ubunifu madhubuti wa njia sahihi za kukabiliana na uhalifu mtandao nchini India.

Waziri mkuu Huyo mhe. Narendra Modi, Ameyazungumza hayo alipokua akizungumza na wana TEHAMA Nasscom, Waziri mkuu huyo alizungumza na kusema dunia nzima imekua ikiangazia macho maswala ya usalama mitandao na kusisitiza toka alipopata wadhfa huo amekutana na wanasiasa takriban 50 na kati yao wanasiasa kati ya 25 – 30 wamekua wakionyesha hisia zao juu la wimbi kubwa la uhalifu mtandao unao kua kwa kasi.

Waziri mkuu huyo akauliza swali, Vijana wa Ki hindi wako tayari kufanyia kazi kupata suluhu la matatizo ya uhalifu mitandao? Huku akiongezea kua maswala ya usalama mitandao yana weza kuongezea sana kipato taifa hilo na kuishauri Nasscom kuangazia swala hilo ili baadae kutoa huduma stahiki za kiusalama mitandao katika mataifa mbali mbali duniani.

Katika kuongezea Waziri mkuu huyo alielezea TEHAMA inauwezo mkubwa sana wa kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya utalii nchini humo. Alitoa changamoto kwa wana TEHAMA wa india kwa kutofaninisha kupatikana kwa Google iliyotengenezwa nchi humo.

Akizungumza na Deccan Herald – Mkurugenzi mkuu wa Happiest Minds Technologies Ashok Soota, Waziri mkuu huyo alionyesha furaha yake kwa sekta ya TEHAMA kuweza kuzalisha Dola za kimarekani Bilioni 146 na kusababisha dunia kuitazama tofauti nchi hiyo.


Taarifa zaidi juu ya Hafla hiyo na aliyo zungumza waziri mkuu huyo unaweza kuyasoma kwa "KUBOFYA HAPA"

No comments:

Post a Comment